Wednesday, October 29, 2008

mfalme wa Nepal akitakiwa umeme kwa madeni



mfalme wa zamani wa Nepal Gyanendra anadaiwa zaidi ya dola za marekani milioni moja (zaidi ya shilingi bilioni moja za Tanzania) na amepewa siku 15 awe amelipa deni hilo la sivyo cha moto atakiona. ukiondoka madarakani mambo ya kunyenyekewa hakuna tena ni undava-undava tu.

kwa habari zaidi fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

utani kwa 'Mungu' atimuliwa Dubai



mmiliki wa radio binfasi revin john raia wa marekani ametimuliwa Dubai baada ya radio yake kuingiza utani wa 'Mungu' kwenye kipindi chake cha comedy kwa kuigiza sauti ya 'mungu' wakidai wanaongea naye kwa simu. utani wowote wa Mungu au Mtume Muhammad ni marufuku Dubai.

Kwa habari zaidi fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

Ban Ki-moon awaasa waandishi wa habari


Na Maura Mwingira,New York-Marekani

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki Moon, ametoa wito kwa waandishi wa habari duniani kote, kuandika habari zinazowahusu watu wanyonge, masikini na wasio kuwa na sauti, licha ya mazingira magumu na vikwazo mbalimbali wanavyokumbana navyo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Alisema UN inatambua mazingira magumu wanayofanyia kazi waandishi wa habari, na amewataka kutokata tamaa.

Mbali na hilo alisisitiza kuwa Umoja wa Mataifa daima utapinga na kukemea vitendo vyovyote vinavyolenga kuathiri utendaji kazi wao.

Katibu Mkuu alitoa wito huo wakati wa chakula maalumu kilichoandaliwa kwa heshima ya waandishi wa habari wanne, ambao wamefadhiliwa na taasisi ya Dag Hammarskjold, kuja Umoja wa Mataifa, kujifunza na kuandika habari za umoja huo.

Miongoni mwa waandishi hao ni Erick Kabendera kutoka Tanzania anayeandikia gazeti la The Citizen. Kabendera anakuwa mwandishi wa tatu kutoka Tanzania kupata ufadhili wa taasisi hiyo, ikiwa ni miaka zaidi ya 20 tangu mwandishi wa mwisho kutoka Tanzania kufanikiwa kupata ufadhili wa taasisi hiyo.

Mwandishi Mwandamizi wa Magazeti ya Serikali (Daily News) Mkumbwa Ali, ni mmoja wa waandishi waliowahi kufanikiwa kupata ufadhili wa taasisi hiyo.

Jumla wa waandishi wa habari 200 walishindania nafasi nne ambapo, Erick Kabendera (Tanzania), Patricia Caycho (Peru),Grevazio Zulu(Zambia) na Ebtihal Mubarak (Saudi Arabia) kazi zao ziliwaridhisha majaji na kuteuliwa kuja Umoja wa Mataifa kupitia Taasisi hiyo ya Dag Hammarskjold.

Ban Ki-moon alisema katika mazingira ya sasa ambapo dunia imekumbwa na changamoto mbalimbali, zikiwamo za kuyumba kwa uchumi wa dunia, ni rahisi kwa wananchi wanyonge na masikini kusahaulika.

Katika hafla hiyo, iliyohudhuriwa pia na mabalozi kutoka mataifa mbalimbali, Ban Ki-moon alisema Umoja wa Mataifa utaendelea kufanya kazi kwa karibu na vyombo vya habari, na kuishukuru taasisi ya Dag Hammarskjold kwa kazi nzuri ya kutoa nafasi kwa waandishi kujifunza utendaji kazi wa kila siku wa Umoja wa Mataifa.

Akisoma taarifa yake iliyowasisimua na kuwagusa wageni waalikwa katika hafla hiyo, Kabendera, alielezea changamoto mbalimbali zinazowakabili watanzania hususan katika nyanja za huduma za afya na elimu.

Kabendera aliieleza hadhara hiyo, kwamba pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na serikali katika kuboresha huduma za afya ili kinamama wajawazito wajifungue katika mazingira yaliyo salama na bora, bado uwezo wa serikali ni mdogo.

I am so sorry to all of you

I am sorry to all of you, I was not in Delhi, I went to Nainital for study tour, now I am back everythings will be under control, worry not my dear. by noor shija.

Wednesday, October 15, 2008

Shushushu wa kike anayetumia ngono akamatwa



Shushushu wa kike wa Korea Kaskazini Won Jeong-hwa, 34, ayetumia mwili wake kwa kufanya ngono na wanajeshi wa serikali ya Korea Kusini, amekamatwa Korea Kusini na kula kifungo cha miaka mitano jela. (kushoto ni ushahidi uliokusanywa na kulia ni Won Jeong-hwa.
kwa habari zaidi fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

serikali Vietnam yamfunga jela mwandishi kwa kuandika habari za rushwa




mahakama ya Vietnam imemfunga jela miaka miwili mwandishi wa habari Nguyen Viet Chien, 56, kisa! kaandika habari za rushwa. (pichani mkewe akilia baada ya hukumu na kulia ni Viet).
Kwa habari zaidi na picha mbalimbali fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

Ubalozi wa Uganda Ubelgiji wageuka makazi ya wavuta unga


Serikali ya Uganda imeamua kulivunjilia mbali jengo la ubalozi wake Ubelgiji kwakuwa limegeuka makazi ya wavuta unga na wahuni. jengo hilo lilinunuliwa na aliyekuwa rais wa Uganda dikteta Idi Amin Dadaa miaka kibao iliyopita. kwa habari zaidi na picha mbalimbali za jengo hilo fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

Afrika 'tamu unapoondoka' madarakani


Mzee mzima Colin Powell akijirusha muziki wa hip-hop wakati wa tamasha la utamaduni wa Afrika lililofanyika jijini London. kwa habari motomoto kuhusu tamasha la Afrika na kujirusha kwa Powell fungua hapa: http://shija.blog.co.in/

Monday, October 13, 2008

kuachana ni ukichaa eti! wagawana nyumba



kuachana wakati mwingine huwa ni ukichaa, tazameni haya maajabu mke na mume huko Cambodia wameamua kugawana kwa kuikata katikati hii nyumba, kila mtu akachukua kipande chake, ama kweli ndoa ndoano, ikishindwa kufanya kazi inazama na mtu. (kulia ni kipisi cha nyumba).

kwa habari zaidi kuhusu hawa wanandoa bonyeza hapa http://shija.blog.co.in/ mambo yote utayapata humo. changamkia tenda mwanangu.

Saturday, October 11, 2008

Dunia ina Mambo

(hii nimeitoa kwenye blog ya Mpoki Bukuku- Mzee wa Sumo) mimi sihusiki nayo ni ya watu wa Mbeya.

(jeneza lenye maiti ya mama lasafirishwa na zawadi ndani yake)


Familia moja ilishangazwa pale walipopokea jeneza la marehemu mama yao aliyefariki nchini Marekani. Lilitumwa na mmoja ya watoto wake wa kike.
Mwili ndani ya jeneza ulikuwa umesongwa sana ndani ya jeneza kiasi kwamba uso wa marehemu ulikuwa umegusa kioo cha jeneza! Walipofungua jeneza, walikuta barua juu ya merehemu, iliyosomeka namna hii:
'Wapendwa ndugu zangu, nimeutuma mwili wa mama yetu kwa ajili ya mazishi, kwani imekuwa siku zote hamu yake kubwa kuzikwa nyumbani Ileje, katika nyumba ya ukoo.
Samahani sikuweza kuja na mwili kwani nimenyimwa likizo kwani kuna upungufu wa wafanyakazi hapa kazini mwezi huu. Ndani ya jeneza, chini ya mwili wa mama, kuna makopo 12 ya samaki wa makopo, paketi 10 za supu ya Royco na chupa 8 za jam ya maembe.
Mgawane hivi kwa jinsi mtakavyoamua nyinyi. Katika miguu ya mama kuna pea moja ya viatu vya Reebok namba 9 kwa ajili ya mtoto mkubwa wa Mwakajinga. Pia, kuna pea mbili za viatu kwa ajili ya watoto wa Mwakipesile na Ipiana , natumaini nitakuwa sijakosea namba za miguu. Nimemvalisha pia mama American T-shirts 6, kubwa kabisa ni kwa ajili ya Mwakibibi, na zinazobaki ni za watoto wake.
Hizo jeans mpya 2 ambazo mama amezivaa ni za wavulana Mwakatumbula na Mwakitobe. Hiyo Swiss watch mkono wake wa kushoto ni zawadi ya Rhoida kwa ajili ya sikukuu yake ya kutimiza miaka 21. Anti Queen, hizo heleni, mkufu na pete ambazo mama amevaa ni zako.
Hizo soksi 6 ambazo mama amevaa wagaiwe wajomba. Tafadhali mgawane kama nilivyosema na kama kuna kitu kingine mnahitaji, basi mnieleze kwani hali ya baba nayo siku hizi si nzuri sana .
Dada yenu mpenzi, Mama Mpoki

Monday, October 6, 2008

ghorofa lanyanyuliwa kwa jeki 275

Ni maajabu lakini ni kweli

Ghorofa lililojengwa kwenye eneo lililotitia na kulifanya lizame kwa futi tano na kuingia maji ndani, limenyanyuliwa kwa kutumia jeki za magari makubwa 275 kwa urefu wa futi 11. aimini usiamini mmiliki wa kampuni hiyo ana elimu ya darasa la nne na watoto wake wanne anaoshirikiano nao wana elimu ya msingi isiyozidi darasa la 10.

kwa habari za undani kuhusu jengo hilo na picha kem kem na namna walivyofanya fungua blog. http://shija.blog.co.in/ pata uhondooo!

Rais wa Pakistan alimlilia mkewe UN


Rais wa Pakistan Asif Ali Zardari alitoa mpya kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa baada ya kuingia na picha ya mkewe marehemu Benazir Bhuttto aliyeuawa kwa bomu na kutaka UN iunde tume huru kufanya uchunguzi. pichani Zardari akionyesha picha yaBenazir.

habari zaidi kuhusu vituko vya Zardari ndani ya UN fungua blog. http://shija.blog.co.in/ utapata mambo kwa kirefu na upana enjoy mambooooozzzzi

'vimini Uganda stop'


vimini Uganda vinaandaliwa mpango wa kupigwa stop, baada ya waziri kudai kuwa vinasababisha ajali kwa madereva kupiga shingo kupita kiasi. kama hiki nadhani ni balaaaa.

:- Kwa habari zaidi za vimini soma http://shija.blog.co.in/ utapa mambo mengi ya kufurahisha, nenda sasa...

Saturday, October 4, 2008

this from Simon Martha Mkina:


Dear all Hope you are doing fine. I am ok.

Iam just informing you that I have been nominated a journalist of the year in Tanzania 2008 (in investigative journalism). Given a certificate and some money. Nomination was done by Media Institute of Southern Africa (Misa), USAID, Pact Tanzania and a number of journalism guru in the country.

Thanks for your cooperation.

--
Simon Martha Mkina,
Editor/Columnist/Author
Dar es Salaam
TANZANIA


0000000000000


KAMANDA WA ZAMANI WA JESHI LA RWANDA KUANZA KUJITETEA MWENYEWE JUMATATU IJAYO



Na Nicodemus Ikonko, Hirondelle,Arusha



Kamanda wa zamani wa Kikosi cha Usalama Jeshini nchini Rwanda , Meja Francois-Xavier Nzuwonemeye anayekabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kimbari katika kesi moja na maafisa wenzake watatu, Jumatatu ijayo atapanda kizimbani kuanza kujitetea mwenyewe mbele ya Mahakama ya Umoja wa Mataifa.



Mashahidi 27 wameshatoa ushahidi wa kumtetea mtuhumiwa huyo wa tatu. Wengine katika kesi hiyo ni pamoja na Makamu wake, Kapteni Innocent Sagahutu atakayefuata katika utetezi baada ya bosi wake kuhitimisha ushahidi wake.



Watuhumiwa wengine wawili ambao tayari wameshatoa utetezi wao mahakamani ni pamoja na aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Rwanda , Jenerali Augustin Bizimungu na Mnadhimu mwingine wa Jeshi la Polisi, Jenerali Augustin Ndindiliyimana.



Kwa mujibu wa Wakili Kiongozi wa mtuhumiwa Nzuwonemeye, Charles Taku kutoka Cameroon , kuna uwezekano wa kuitwa kwa mashahidi zaidi katika kesi hiyo wakiwemo wawili ambao tayari wameshaandaliwa wanaotambulika kwa majina bandia ya ‘FK’ na ‘B2’ kwa ajili ya usalama wao.



Mahakama namba II inayosikiliza kesi hiyo Septemba 22, 2008 ilitoa onyo kwa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama hiyo, Hassan Bubakar kwa kushindwa kuwapatia mawakili wa utetezi katika kesi hiyo baadhi ya nyaraka za ushahidi wa maandishi kama inavyotakiwa katika sheria iliyoanzisha mahakama hiyo.



Kwa mujibu wa Wakili Taku, tayari mwendesha mashtaka huyo ameshawapatia nyaraka tatu za ushahidi wa maandishi mawakili wa timu za utetezi kutoka katika majalada ya Kundi la zamani la Waasi nchini Rwanda (RPF).



Kesi hiyo ilianza kuunguruma mahakamani tangu Septemba, 2004



0000000000000000

Kuwe makini na Mitandao- Wanafunzi waambiwa

NA SOLOMON MWANSELE,MBEYA.

WAHITIMU wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ST.Mar's Mbeya, wametakiwa kuzitumia Intaneti kwa kujisomea zaidi, badala kuangalia picha ambazo hazina maadili mazuri kwa jamii.

Imeelezwa kuwa wanafunzi wengi hivi sasa wamekuwa na tabia ya kutumia muda mwingi intaneti wakiangalia picha hizo, hali inayochangia kuwapotosha maadili.

Changamoto hiyo imetolewa na Ofisa Tawala wa shule hizo mkoani hapa, Anuciatha Ngonyani, wakati wa mahafali ya kwanza ya kidato cha nne yaliyofanyika shuleni hapo.

Jumla ya wahitimu 48 wakiwemo wavulana tisa, walitunukiwa vyeti vyao vya kuhitimu na Ofisa Afya wa halmashauri ya jiji la Mbeya Dk.Mathias Kapizo.

Ngonyani alisema wakiwa shuleni hapo wahitimu hao wamefundishwa pia maadili mema na hivyo kuwataka kutojiingiza katika makundi ya utumiaji wa dawa za kulevya na uhuni, kwani watakuwa mfano mbaya katika jamii.

Alisema wanakwenda kwenye ulimwengu wa utandawazi ambao hivi sasa dunia ni sawa na kijiji kimoja, hivyo kuhakikisha kuwa wanajiendeleza zaidi na siyo kuishia kidato cha nne.

"Tumieni elimu mliyoipata mkiwa hapa shuleni kwa miaka minne kwa kujiendeleza zaidi kielimu huko muendako...Msipende kuzitumia Intaneti kwa kuangalia picha za ngono bali kujisomea zaidi" alisema.

Naye mgeni rasmi Dk.Kapizo alisema wahitimu hao wanatakiwa kuwa kioo kwa vijana wengine ambao hawajaweza kupata elimu kama waliyoipata yao licha ya kuwa nao wanatakiwa kujiendeleza zaidi.

Dk.Kapizo alisema:"Nidhamu ni kitu cha kwanza , pili mnatakiwa kuondoa hofu mtakapoingia chumba cha mtihani kwani mtakutana na yale yale mliyofundishwa na walimu wenu hapa shuleni".

Aliongeza kuwa hakuna mitihani inayotungwa nje ya silabasi, lakini wengi wao huwa wanafeli kutokana na kuwa na uoga wanapoingia katika chumba cha mtihani hali inayopelekea washindwe kufanya vizuri mitihani.

Kwa upande wao wahitimu hao wakisoma risala yao kwa mgeni rasmi, waliiomba serikali kutoa ruzuku kwa shule za binafsi katika baadhi ya vifaa kama vitabu na vifaa vingine vya maabara.

Walisema endapo serikali itafanya hivyo, itatoa changamoto kubwa kwa baadhi ya wanafunzi kusomamasomo ya sayansi hivyo kuongeza idadi ya wataalamu katika sekta ya afya na nyinginezo zinazotokana na masomo hayo.


0000000000000


vijimambo vya ndani ya nchi

Watoto waliokufa Tabora watajwa


* Rais Kikwete, CCM watuma rambirambi
* NSSF yatoa ubani 500,000/- kwa kila familia

Na El - hadji Yuusuf, Tabora

MAJINA ya watoto 19 waliokufa kwa kukosa hewa katika ukumbi wa disko mjini hapa, wakati wa kusherehekea sikukuu ya Idd el-Fitri juzi, yametajwa.

Wakati majina hayo yakitajwa, Rais Jakaya Kikwete, ametuma rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora na wazazi wa watoto hao.

Watoto hao walianguka baada ya ukumbi wa Bubbles Night Club na Oneten Disko Teck, katika maghorofa ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kutokuwa na hewa ya kutosha, hivyo kusababisha vifo na wengine kujeruhiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa, alisema tukio hilo limeshitua wengi na kwamba limeleta hali ya fadhaa kwa wazazi na walezi.

Aliwataja watoto waliopoteza maisha katika tukio hilo kuwa Veronica Maningu, Beatrice Makelele, Jacob Gerald, Salma Hamis, Hadija Waziri, Rehema Moyo, Seleman Idd, Mrisho Seleman, Abdallah Rehani na Agatha Maningu.

Wengine waliopoteza maisha ni Paulina Emmanuel, Ramla Yenga, Mohamed Kapaya, Habiba Shaaban, Donald Kasela, Mwanahamisi Waziri, Philipo Haule, Ashura Jamal na Yassin Rashid.

Mwinyimsa aliwataja watoto waliozimia na kulazwa katika hospitali ya mkoa wa Tabora ya Kitete kwa matibabu kuwa, Sakina Ali, Daudi Chape, Shufaa Azan, Naomi Joseph, Amani Emilian, Jumanne Mashaka, Kulwa Iddi, Msimu Rehani, Bahati Hamisi na Bertha Maneno.

Wengine waliolazwa ni Asia Mohamed, Mwami Masumbuko, Shida Kassim, Kenea Masudi, Agness Kasele, Josephine Julius, Tatu Hamad na Ramadhani Idd.

Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili jana, Kaimu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Tabora, Daudi Siasa alisema watoto 10 waliruhusiwa kutoka hospitalini jana, huku sita wakiendelea na matibabu.

Kutokana na tukio hilo, Mwinyimsa alisema serikali kupitia vyombo vya usalama, imeanza kuchukua hatua madhubuti baada ya kuwakamata watu waliokuwa wakipiga disko katika kumbi za Bubbles na Oneten katika jengo la NSSF yalikotokea maafa hayo.

Mbali na kukamatwa kwa watu hao, alisema serikali imeunda tume itakayofanya kazi kwa siku saba kuchunguza chanzo cha tatizo hilo.

Alisema tume hiyo itahusisha watu kutoka idara za ujenzi, Jeshi la Polisi na usalama wa taifa na inatakiwa kuwasilisha taarifa wiki ijayo.

Mwinyimsa alisema serikali itagharamia maziko ya watoto hao, na kutoa ubani wa sh. 50,000 kwa kila mzazi, ikiwa ni pamoja na kupendekeza watoto hao wazikwe mahali pamoja kwa ajili ya kuweka kumbukumbu rasmi.

Kwa mujibu wa watoto walionusurika katika ajali hiyo ndani ya kumbi hizo za starehe zilizo katika eneo moja, kulikuwa na joto kali na kulikuwa na harufu mbaya.

Walisema hali hiyo ilisababisha takriban watoto 50 kuanguka, ambapo 19 walikufa.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete ametuma rambirambi na kutuma ujumbe maalumu utakaoongoza shughuli za maziko zinazotarajiwa kufanyika mjini Tabora.

Ujumbe huo utaoongozwa na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya.

Rais alisema amepokea kwa mshituko mkubwa habari za vifo vya watoto hao na amehuzunishwa na kusikitishwa na msiba huo.

“Nimepokea kwa mshituko mkubwa, huzuni nyingi na masikitiko yasiyokuwa na kifani habari za vifo vya watoto hao wasiokuwa na hatia, ambao walikuwa wanasherehekea sikukuu ya Idd el Fitri kama tulivyokuwa tunafanya sisi sote,” alisema Rais.

Aliongeza: “Mawazo yangu yote yako kwa wazazi na wanafamilia wa watoto hao katika kipindi hiki kigumu cha huzuni, majonzi na msiba mkubwa. Tunawaombea kwa Mwenyeji Mungu waweze kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu”.

Rais Kikwete alisema ni matarajio yake kuwa, vyombo vya sheria vitachunguza kikamilifu na ipasavyo vifo vya watoto hao na kuchukua hatua zinazostahili.

Kwa upande wake, Profesa Kapuya akitoa salamu za Rais, aliuambia umati uliokusanyika katika hospitali ya Kitete mjini Tabora kwa ajili ya kuchukua miili ya marehemu hao, kuwa NSSF itatoa ubani wa sh. 500,000 kwa kila familia iliyopoteza mtoto.

Wakati huo huo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa rambirambi kutokana na vifo hivyo.

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa Halamshauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati, ilisema Chama kinaungana na serikali na wazazi wa watoto waliopoteza maisha katika kipindi hiki kigumu.

Chiligati alisema ni vyema wananchi, hususan wazazi wa watoto hao kuwa na subira wakati huu, ambapo tume iliyoundwa inachunguza chanzo cha tatizo hilo


00000000000000

• Ni simanzi tu Tabora


* Baadhi ya watoto wazikwa
* Karume atuma rambirambi

Na El - hadji Yuusuf, Tabora
WAZIRI wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, jana aliwaongoza mamia ya wakazi wa Tabora, katika mazishi ya watoto 19 waliokufa kwa kukosa hewa wakiwa kwenye kumbi za disko kusherehekea sikukuu ya Idd el Fitri.

Mazishi ya watoto hao yalifanyika kwenye maeneo mbalimbali, Profesa Kapuya, ambaye alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete, alihudhuria ya watoto wanne.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi ya watoto hao ni Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki, mkoani humu na mkewe, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Margaret Sitta, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu.

Wengine ni Mkuu wa mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau. Maafa hayo yalitokea kwenye jengo la shirika hilo.

Profesa Kapuya, ambaye ni Mbunge wa Urambo Magharibi, alihudhuria mazishi ya watoto hao, waliozikwa katika maeneo ya Ng’ambo na Rufita.

Spika Sitta alihudhuria kwenye mazishi ya watoto wawili yaliyofanyika eneo jirani na uwanja Ali Hassan Mwinyi.

Watoto hao walikubwa na maafa hayo Jumatano wiki hii, wakiwa disko kwenye kumbi za Bubbles Night Club na Oneten Disco Theque.

Watoto 16 walijeruhiwa, ambapo hadi jana wanne bado walikuwa wakiendelea na matibabu kwenye hospitali ya mkoa ya Kitete.

Kwa mujibu wa Mwinyimsa, hali za watoto hao zinaendelea vizuri, licha ya kukaa muda mrefu bila ya kupata fahamu.

Aliwashukuru wananchi kwa kuwa watulivu tangu mkasa huo ulipotokea na kwa ushirikiano waliouonyesha katika kipindi hiki kigumu.

Akizungumzia kuhusu tume aliyoiunda kuchunguza tukio hilo, alisema inaanza kazi leo.

Alisema moja ya mambo ambayo yanatarajiwa kupatiwa ufumbuzi na tume hiyo ni kujua kama wafanyabiashara wa kumbi hizo walifuata sheria na taratibu, kama kumbi hizo zilikuwa na nafasi ya kutosha na vifaa vya tahadhari.

Mwinyimsa alisema tume hiyo itawahoji watu muhimu na wale ambao wataonekana kuwa na uwezo wa kutambua kilichojiri katika ukumbi huo, wakiwemo watoto walionusurika.

Aliwataja watu wengine ambao tume hiyo inatarajiwa kuwahoji kuwa, wamiliki wa kumbi hizo, mameneja, wazuia fujo katika kumbi hizo na watu wengine watakaojitokeza, ambao wanaweza kuipa ushirikiano tume kufanyakazi vizuri.

Mwinyimsa alisema polisi inawashikilia Shashikant Patel, mkurugenzi wa Bubbles Night Club na meneja wake Vituko Salala.

Wengine ni Mkurugenzi wa Oneten Disco Theque, Projestus Fidelis ‘Porojo’ na meneja wake, Jaffar Rashid.

Alisema walinzi wa milangoni waliokimbia baada ya tukio hilo, wanaendelea kusakwa na polisi.

Kwa mujibu wa Mwinyimsa, serikali itachukua hatua dhidi ya watakaobainika kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kusababisha tukio hilo.

Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, ametuma rambirambi kwa wananchi wa Tabora kutokana na vifo hivyo.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, Rais Karume alieleza kushtushwa na vifo hivyo, vilivyohusisha watoto wadogo wasio na hatia.

Alisema taifa limepata hasara kuwapoteza watoto, ambao ni matumaini ya wazazi na taifa.

Katika hatua nyingine, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, imetuma rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa watoto waliofariki dunia katika tukio hilo.

Rambirambi hizo zilitolewa jana na wizara kupitia Msemaji wake Erasto Ching'oro, aliyesema wizara imepokea kwa masikitiko makubwa na kwamba msiba huo ni wa taifa.

Wakati huo huo, Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), kimetoa pole kwa familia za watoto hao, na kuitaka serikali ichukue hatua kuhakikisha viwanja vya michezo na burudani vilivyoporwa na matajiri vinarejeshwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho, Ananilea Nkya, alisema wamekuwa wakifuatilia na kubaini katika miaka ya hivi karibuni maeneo mengi yaliyokuwa yametengwa kwa ajili ya michezo yamegeuzwa viwanda vidogo, gereji, baa, migahawa, maduka, hoteli na vituo vya mafuta.


000000000000000

• Uchunguzi makini ufanyike vifo vya watoto Tabora


MAONI……

MARA kwa mara, wakati wa maadhimisho ya sikukuu, limekuwa jambo la kawaida kuripotiwa watu kufa katika ajali za barabarani na wengine kupigwa kutokana na ugomvi, hususan kwenye maeneo ya starehe.

Katika maadhimisho ya sikukuu ya Idd el-Fitri yaliyofikia kilele juzi, pia kumeripotiwa kutokea mambo mbalimbali katika sehemu mbalimbali hapa nchini yakiwemo ya watu kupoteza maisha.

Licha ya kuwepo mambo mengi, kubwa zaidi ni la kupoteza maisha kwa watoto 19 kwenye ukumbi wa disko huko Tabora. Hayo ni maafa makubwa na ya kutisha.

Imeripotiwa kuwa watoto hao, wanane wakiwa wavulana na 11 wasichana, walikufa kutokana na kukosa hewa katika ukumbi wa disko wa Bubbles,na oneten,zilizoko katika jengo linalomilikiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa, watoto waliokufa wanakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka saba na 18. Wengine 16 walilazwa katika hospitali ya mkoa, watatu hali zao zikiwa mbaya.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa watoto hao walijaa kupita uwezo wa ukumbi, jambo lililosababisha mzunguko wa hewa kuwa mdogo.

Wakurugenzi kadhaa wa ukumbi huo imeelezwa wanashikiliwa na polisi kwa kuhojiwa kuhusu tukio hilo la kusikitisha.

Mwinyimsa alisema kamati imeundwa kuchunguza tukio hilo, ikihusisha maofisa kutoka Polisi, Usalama wa Taifa, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Tukio hilo linaonyesha wazi kwamba, wenye ukumbi hawakuwa makini katika kusimamia shughuli hiyo.

Ni jambo lililo dhahiri kwamba walijali zaidi maslahi binafsi, badala ya afya za walioingia kwenye ukumbi huo.

Katika msongamano huo, licha ya waliopoteza maisha, kuna uwezekano mkubwa wa baadhi ya watoto hao kuambukizwa maradhi yanayoenezwa kwa njia ya hewa.

Wakati tunaungana na familia za watoto waliopoteza maisha, tungependa kushauri mambo kadhaa juu ya hatua ambazo tunadhani zinafaa kuchukuliwa.

Kwanza, tume iliyoundwa kuchunguza maafa hayo ifanye kazi kikamilifu na umakini mkubwa, ili matokeo yatoe picha halisi ya chanzo chake.

Pili, kwa kuwa uchunguzi unahusisha vyombo vya dola basi endapo itabainika kuwepo uzembe kwa upande wowote hatua stahiki zichukuliwe kwa waliohusika.

Tunasema haya kwa sababu hatuamini kwamba watoto wanaweza kujaa kwenye ukumbi kiasi cha kukosa hewa bila tahadhari yoyote ya madhara ambayo yangeweza kutokea.

Hivyo katika uchunguzi huo, ni vyema jengo hilo likachunguzwa ujenzi wake, na ikibainika haukuzingatia taratibu na halifai kwa shughuli za disco wahusika wawajibishwe.

Kwa kifupi mamlaka husika zinapaswa kuchukua hatua madhubuti kwa wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo, ili lisijirudie katika siku zijazo.


00000000000000000

Mgombea ugavana amtwanga mwandishi


BANGKOK, Thailand

MMOJA wa wagombea ugavana wa jiji la Bangkok juzi alimshambulia kwa ngumi na mateke mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni kwa madai ya kukerwa na maswali magumu.

Mgombea ugavana huyo, Chuvit Kamolvisit alikuwa akiulizwa na mwandishi huyo, huku mahojiano hayo yakirushwa moja kwa moja.
Hata hivyo, mgombea huyo aliomba radhi, akisema alipandwa na ghadhabu baada ya kuona kuwa maswali ya mwandishi huyo, Visam Dilokwanich, yanalenga kumuumbua ili anyimwe kura kwenye uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika kesho.

“Nakiri nilifanya hivyo. Sikuvumilia kwa kuona ananiumbua moja kwa moja kupitia televisheni,” alisema Chuvit, mtu wa miraba minne aliyewahi kumiliki baa kadhaa jijini Bangkok, zenye wahudumu wanaovalia vivazi vya nusu uchi.

“Nilichofanya ni uhalifu, na ni haki kwangu kulipa faini kwa kumdunda kwa ngumi na mateke,” aliongeza Chuvit, ambaye hana nafasi kubwa ya kushinda kwenye uchaguzi huo.
Mwanahabari huyo alifungua kesi polisi, akisema Chuviot alionekana kama jambazi.

“Alikasirika sana nilipomwambia kwamba alichokuwa akisema katika mahojiano hayo yalikuwa tofauti sana na anachokisema akiwa sehemu nyingine,” alieleza Visarn, akiwaonyesha wanahabari wenzake majeraha aliyopata shingoni na kichwani baada ya kipigo.


00000000000000

• Ndege tano zaporwa Mexico


MEXICO CITY, Mexico

WATU wenye silaha juzi walipora ndege tano ndogo kutoka kwenye uwanja binafsi, katika mji wa Kaskazini Magharibi mwa Mexico wa Sinaloa, baada ya kumzidi nguvu polisi.

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, waporaji hao, wanaokadiriwa kufikia 20, walivamia uwanja huo mdogo wa ndege alfajiri, wakamnyang’anya polisi bunduki, wakamfunga kamba, wakajaza mafuta katika ndege hizo, na hatimaye wakaruka.

Msemaji wa kikosi cha polisi kinachopambana na mtandao wa kihalifu, Emma Quiroz alisema kuwa haikufahamika iwapo kuna uhusiano kati ya waporaji hao na genge linalojihusisha na dawa za kulevya aina ya ‘cocaine’.

Kundi hilo kwa kawaida hutumia ndege ndogo kusafirisha dawa hizo Kaskazini mwa Mexico hadi mpakani na Marekani.
Alieleza kuwa polisi wanachunguza iwapo uporaji huo ulifanikishwa kwa msaada wa baadhi ya maofisa serikalini.

Taarifa ilieleza kuwa vyombo vya usalama vilikuwa vikifuatilia kujua wapi ndege hizo zimepelekwa, na pia kuwakamata waporaji. Alisema ziliporwa eneo la kufanyia matengenezo kwenye uwanja huo unaomilikiwa na kampuni ya kunyunyizia dawa mazao ya kilimo mjini Navolato.

Jeshi lilizisimamisha ndeghe hizo kutoa huduma mapema mwaka huu, kwa maelezo kuwa hazikuwa katika hali nzuri ya kukidhi usalama wa anga.

Jeshi la ulinzi, ambalo pia linashiriki kukabiliana na genge la dawa za kulevya nchini Mexico, na hasa kwenye majimbo ya Kaskazini, limeshakamata ndege ndogo 245, zikiwemo helikopta, tangu Novemba, mwaka jana.

Sinaloa ni moja ya majimbo ambako magenge yanayojihusisha na biashara ya dawa za kulevya yanakabiliana vikali na jeshi, ambalo kwa mwaka huu pekee limeua watu wapatao 3,000. Ndege ndogo hutumiwa kihalali kunyunyizia dawa mazao mashambani, na vilevile kuteketeza kilimo cha bangi.


00000000000000

Monday, September 29, 2008

Muheshimiwa Cobra ndani ya ndege


Honorable Snake inside plane

An Indian flight to Mumbai was grounded at the airport recently after the crew spotted an unexpected guest on board, that is ‘honorable’ Cobra.

Though there have been instances of reptiles moving around the airport, this is for the first time a snake has managed to sneak into an aircraft.

The snake was found inside a domestic aircraft that had arrived from Srinagar. Airline staff on maintenance duty found the snake below a seat.

“There was commotion which scared the snake and it went further inside,: said an airport source. The snake crawled inside a small air vend below the seat after which the staff opened all doors and unscrewed panels.

The airline informed the airport authorities, who called the NGO Wildlife SOS. But the snake remained untraceable. “the plane was fumigated but it seems the snake went further inside the aircraft,” he said.

The snake was found despite repeated checks. “The plane was already late for the Mumbai flight and a spare plane had to be used,” the source said.
-----------

Hindustan Times of Thursday, September 4, 2008

si kila mtumia net ni mpenda ngono


She thinks I watch porn because I surf the net!

heshima kwa watoto ni busara


Baadhi ya kina mama wanapokosa heshima kwa marafiki wa kiume wa mabinti zao...kama huyu mama!

Saturday, September 27, 2008

mambo ya wakubwa

Mmetonaaaaaa wajemeniiii!!!!!!!!




Mama wa shoka Condeleezza Rice akiwa kwenye tizi hakuna mchezooooo!





Hapo safi mama




Zoezi la baiskeli lina raha yake



Kuoga ni muhimu sana



Nadhani hii habari ina ukweli!



Unasema...?



00000000000000000


UN yataka serikali za mitaa ziwezeshwe

Na Maura Mwingira, New York- Marekani

NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, amesisitiza wajibu wa serikali za mitaa katika kufanikisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya milenia (MDG).

Alisema wajibu huo unatokana na ukweli kwamba, chombo hicho ndicho kilicho karibu zaidi na wananchi, ambao ndio walengwa wa MDG.

Dk. Asha- Rose alisema bila ya juhudi za makusudi zitakazozishirikisha serikali za mitaa kuanzia ngazi ya kata, kijiji, wilaya, miji na mikoa, mafaniko yaliyokwisha kupatikana yanaweza kurudi nyuma.

Naibu Katibu Mkuu huyo alikuwa akifungua mjadala kuhusu wajibu na ushiriki wa serikali za mitaa katika utekelezaji wa MDG, ulioandaliwa na serikali ya Italia na kufanyika makoa makuu ya Umoja wa Mataifa.

Mijadala kadhaa ilifanyika jana kuhusu malengo ya milenia, ikifunguliwa na Dk. Asha-Rose; Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Baraza Kuu la 63 la Umoja wa Mataifa, Miguel D’Escoto.

Ahadi ya dola za Marekani bilioni 16 ilitolewa na makundi mbalimbali ya kijamii, zikiwamo taasisi za fedha, wafanyabiashara, nchi wahisani na watu maarufu katika mijadala hiyo.

Dola za Marekani bilioni 1.6 zimetolewa kwa ajili ya usalama wa chakula, dola bilioni 4.5 kwa mpango wa kuendeleza elimu na zingine kwa ajili ya kupamba na malaria.

Kwa mujibu wa Dk. Asha-Rose, ili serikali za mitaa ziweze kutekeleza majukumu yake vizuri, ni muhimu kuwapo kwa utashi wa kisiasa katika kuziwezesha.

“Serikali za mitaa ndizo zinazotoa dira na mwelekeo wa maisha ya wananchi… zinaendesha vituo vya afya na zahanati, shule na kutoa hudumu muhimu kama za majisafi na majitaka.

“Ni lazima tuzisaidie halmashauri hizi ziweze kuzikabili changamoto na kupata nguvu na uwezo wa kutekeleza majumu yake,” alisema.

Dk. Asha-Rose alisema ingawa uwajibikaji wa jumuia za kimataifa ni muhimu katika upatikanaji wa fedha na utaalamu, bado wajibu wa serikali za mitaa katika kufanikisha malengo ya milenia unahitajika.


000000000000000000000000000

Athari za utani wa ‘mchumba’ kwa wasichana

* Mmoja apata mimba na kutelekezwa

NA JANE MIHANJI

JANDO na Unyago ni mila zilizokuwepo zamani ambazo zilikuwa zikiwafundisha vijana maadili mema na jinsi ya kuishi katika jamii.

Kwa mabinti ambao walikuwa wamebalehe hawa waliitwa na mabibi au mashangazi na kupewa mafunzo maridhawa ya maisha kwa jumla. Ikiwa ni pamoja na usafi wa mwili, upendo, uvumilivu, kujituma katika ufanyaji kazi na suala zima la heshima kwa mkubwa na mdogo.

Halikadhalika jando kwa wanaume. Hawa walipelekwa porini kwa makundi yenye umri wa rika moja huko pamoja na kutahiriwa, basi hufundishwa mambo mengi ikiwemo kuwa mioyo ya ujasiri. Tena wakati huo walikuwa wakiingizwa suna bila hata ganzi.

Siku hizi maadili hayo yanapotea, usasa unawaingiza mabinti wa kike kwenye mambo ya ajabu. Vitu kama kitchen party kwa walio wengi ni kufanya mambo ya kishangingi, kuonyesha viungo vyao na michezo ya ajabu.

Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakidiriki kuwafundisha mabinti hawa kuwa ni lazima kuwa na mafiga matatu kwani moja haliwezi kuinjika chungu.

Hivi karibuni baadhi ya waandishi wa habari kutoka chama cha Waandishi wa habari za ukimwi na afya (AJAAT) walitembelea wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani na kukutana na baadhi ya mambo ambayo pengine yamesababisha na watoto kutoelezwa bayana madhara ya mambo fulani katika maisha.

Selina (siyo jina halisi) ni binti ambaye alipata mimba bila kujua. Akiwa na bibi yake aliweza kusimulia jinsi alivyopata ujauzito huo aliokuwa hajaupanga.

“Kuna kaka alikuwa akinitania na kuniita mchumba, utani huo uliendelea na alikuwa akinipa vitu vidogo vidogo. Wakati wa sikukuu nilimfuata na kumwomba aniletee zawadi huku nikimwuliza kama kweli atanioa.

“Akaniambia ukitaka nikuoe nipe kidogo nionje.Aliniingiza chumbani kwake na nikafanya naye tendo la ndoa. Alikuwa ni mwanaume wa kwanza na siku hiyo hiyo nilipata mimba,” anasema Selina.

Siku zilivyozidi kwenda alikuwa akijisikia homa za hapa na pale, hadi bibi yake alipokuwa kugundua kwamba ana mimba.

Selina akuwahi kwenda kliniki kuangalia afya yake na hali ile ya ujauzito. Siku moja aliamka asubuhi na kusikia amebanwa na haja. Aliingia chooni na kutaka kumaliza matatizo yake, alipojaribu kujikamua aliona hakuna kitu, aliendelea kukaa chooni na baadaye kusikia kitu kizito kikichoropoka na kusikia mlio.

Kumbe alikuwa amejifungua mtoto wa kiume, alianza kulia na kupiga mayowe, majirani walifika na kumsaidia ambapo mtoto yule aliokolewa. Yaliyomkuta Selina ni kupelekwa katika kituo cha polisi na hatimaye mahakamani kwa kujibu mashitaka ya kutaka kuua.

Wakati huo Selina alikuwa na umri wa chini ya miaka 18. Swali la kujiuliza ni kwamba nani alimfundisha Selina hatari ya tendo la kujamiiana? Nani alipata fursa ya kumweleza dalili za hatari kwa mama mjamzito, au dalili za kutaka kujifungua. Hakuna.

“Jando na Unyago ilijumuisha pia suala zima la mahusiano ya kimwili na elimu ya uzazi pia,” anasema Mustapha Selemani na kubainisha kuwa katika suala zima ya elimu ya afya ya uzazi, wazee walikuwa wakitumia zaidi mbinu za kienyeji kwa maada ya kutumia wakunga wa jadi.

Anasema ilikuwa ni jambo la kawaida wazee kuzalisha mabinti zao nyumbani na hakukua na haja ya watu kwenda hospitali, kwanza kutokana na kuwa mbali na vituo vya afya.

Selina kama mabinti wengine wengi, alikosa elimu ya afya ya uzazi. Magreth Shoo ambaye ni muuguzi anasema kuwa ni vema elimu hiyo ikawa inatolewa shuleni.

“Kuna taasisi mbalimba mbali na vyama vya kijamii siku hizi vimekuwa vikianzisha klabu katika shule mbalimbali za sekondari na kuzungumza na wanafunzi juu ya afya ya uzazi, ukimwi na mambo mengi ambayo chanzo huwa ni mahusiano kati ya wanaume na wanawake,” alisema Magreth.

Hussein Yahya, fundi viatu mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam anasema kuwa tabia ya kuzoesha watoto au kuwatania kuita mchumba ni mbaya sana na jamii ikemee.

“Wanaume watu wazima ndiyo wanatabia hii, binafsi siipendi kabisa, mchumba mchumba mwisho inaa mchumba, nimeshashuhudia matukio ya utani wa namna hiyo na baadaye kutokea kwa madhara,” anasema Yahya.

“Akina mama ambao mara nyingi ndiyo huwa na watoto, wakatae tabia hii kabisa siyo nzuri hata kidogo…kwanza mtoto unapomwita hivyo unampa mtihani wa kutaka kujua nini maana ya mchumba, kazi hapo ndiyo inapoanza akija kufahamu, mimi nikisikia mwanangu anaitwa mchumba, huyo mtu tutapambana naye kwasababu nimeshakutana na matukio ya namna hii ambayo baadaye huleta madhara,” aliongeza.

Kwa upande wake, Selina anasema aliona kama ananyanyaswa na kitendo cha kupelekwa polisi na hatimaye mahakamani. Kwani yeye ndiye alikuwa anajua ukweli kwamba hakuwa na nia ya kutaka kumwuua mtoto yule.

“Lakini namshukuru mwanasheria mmoja niliyempata kupita shirika moja la haki za binadamu Dar es Salaam ambaye alinisaidia na nikaachiwa huru. Kwani awali nilikuwa rumande na mtoto. Baadaye nikaachiwa kwa dhamana lakini baadaye kesi haikuendelea,” anasema.

Pamoja na kwamba Selina alibebeshwa mzigo huo mzito na mwanaume, katika tabu zote na misukosuko aliyoipata alijikuta yuko peke yake. Kijana yule alimaliza uhusiano na Selina baada ya kugundua tu kwaba Selina yu mjamzito.

Alimkatisha masomo yake ya elimu ya msingi. Hakuweza kuchukuliwa hatua zozote. Anasema wakati ule hamasa za kuwatia jela wanaopa mimba za wanafunzi hazikuwepo.

Analalamika jinsi maisha yake yalivyokuwa magumu na kusema kuwa asingepata mimba na kuacha shule, pengine angekuwa na maisha mazuri kidogo kuliko ya hivi sasa anayoishi bila kazi.

Selina anasema baada ya kukumbwa na mkasa huo, hapendi kuona mwanamke ananyanyasika au kupata matatizo yanayosababishwa na wanaume.


000000000000000



Watuhumiwa wa ugaidi wabambwa kwenye ndege


* Ni kwa tuhuma za kutaka kufanya ugaidi

COLOGNE, Ujerumani

MAKOMANDO wa Ujerumani wamewakamata watu wawili waliokuwa wanasakwa kwa tuhuma za ugaidi, katika ndege ya KLM iliyokuwa ikijiandaa kuruka kutoka jijini hapa.

Kwa mujibu wa Polisi, watu hao wawili, raia wa Somalia na mwingine msomali aliyezaliwa Ujerumani, inadaiwa walikuwa wakijiandaa kufanya mashambulizi, na wamekamatwa baada ya kufuatiliwa kwa miezi kadhaa.

Ofisa wa Polisi aliieleza televisheni ya hapa, kuwa watu hao walikuwa wakijiandaa kuendesha 'vita vitakatifu', na kwamba taarifa za mipango hiyo zilikutwa nyumbani kwao.

Ndege hiyo ya KLM ilikuwa ikijiandaa kwenda Amsterdam, Uholanzi.

Msemaji wa Jeshi la Polisi,Frank Scheulen, alisema makomando walipanda kwenye ndege hiyo ilipokuwa inakaribia kuruka na kuwakamata watu hao.

Baadaye abiria wote waliamriwa kushuka kwenye ndege hiyo kwa ajili ya kukagua mizigo, kabla ya kuruhusiwa kuruka saa moja baadaye.Ndege hiyo ilitua salama Amsterdam.


00000000000

Kuna mchanga unaohama Ngorongoro


AMA kweli kutembea ni kuona mengi, ndivyo tunavyoweza kusema. Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vya utalii ambavyo wengi wetu hatuvijui.

Katika Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro (NCAA) iliyoko mkoani Arusha kuna mchanga unaohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa wastani mita 100 kila mwaka.

Mchanga huo umejikusanya mithili ya kichuguu, na ‘husafiri’ kutoka mahali unapokuwa kwenda mashariki mwa hifadhi hiyo.

Kwa sasa, mchanga huo uliopewa jina la kiingereza la ‘moving sand’ uko takribani kilometa 40 kutoka mahali yalipo makumbusho ya Oldupai (Olduvai) ndani ya hifadhi hiyo.

Pamoja na maajabu hayo ambayo yalibainishwa na watafiti wa mambo ya kale waliokuwa wakifuatilia jinsi binadamu wa kale alivyoishi, waligundua pia kwamba huwa hauchani.

Badala yake, husafiri jinsi ulivyo bila kuacha chembe nyuma. Kwa miaka mingi umekuwa kivutio kikubwa cha watalii wanaotembelea eneo la hifadhi.

Watafiti wanasema, aina hiyo ya mchanga hupatikana karibu na ziwa Manyara, lililoko nje kidogo ya hifadhi hiyo.

Wamasai ambao ni miongoni mwa makabila yanayoishi ndani ya hifadhi hiyo huutumia kutoa kafara na kufanya matambiko mbalimbali.

Matambiko hayo hufanywa ili wapate ‘baraka’ kutoka kwa Mungu na pia kuzaa watoto wengi kwa jinsi wanavyopenda. Ili kufanikisha matakwa yao, huchinja wanyama tofauti kama sehemu ya tambiko.


000000000000

Maradhi ya upotevu wa kumbukumbu


BAADHI ya watu wanapofikia umri wa uzeeni hukabiliwa na maradhi ya kupungua uwezo wa kuweka kumbukumbu na hata kuchanganua mambo.

Mazingira ya namna hiyo huweza kuwapata pia baadhi ya watu, bila kujali kuwa wamefikia katika umri huo wa uzee.

Wakati mwingine, mtu mwenye maradhi ya namna hiyo, waweza kudhani ni mwehu, kwa sababu kwa sababu wakati unazungumza naye, anaweza kutamka ghafla jambo ambalo ni kinyume kabisa ama halihusiani na mada mnayozungumzia.

Kwa maneno mengine ya mitaani, vijana husema kuwa mtu wa namna hiyo anapoteza ‘network’.

Haya ni maradhi ambayo yamekuwa yakiwasumbua wengi japokuwa pale yanapotokea kwa wazee, huyachukulia tu ni hali ya uzee.

Wanasayansi wanasema kuwa inapokuwa siyo uzee basi maradhi hayo yanaweza kuoanishwa na ajali ambayo mtu aliipata katika historia ya maisha yake.

Wanasayansi wanasema haya siyo maradhi ambayo mtu anazaliwa nayo bali humtokea akiwa tayari ameanza kuishi.

Kwa kawaida tatizo hilo huanza kwa mtu polepole kupoteza kumbukumbu ikifuatiwa na mtu kushindwa kufanya kazi ambazo kawaida zilikuwa ndani ya uwezo weke.

Hatua inayofuatia anakuwa anachanganya mambo, mathalan ulikuwa umeshinda naye siku nzima anakuuliza, umerudi saa ngapi?
Wewe utashangaa kwanini akuulize hivyo wakati wote mlikuwa pamoja.

Mtu wa namna hiyo pia akienda mahali huweza kusahau njia ya kurudi nyumbani japokuwa inawezekana kabisa alizaliwa na kukulia mazingira yao.

Katika hatua nyingine atapoteza kabisa mawasiliano na hata uwezo wa kujitambua kiasi kwamba hata kama yu uchi hatakuwa na ufahamu wa kujisetiri. Maradhi haya ni tofauti na wehu au utimbio wa ubongo.

Lakini, wanasayansi wanaamini pia kuwa maradhi haya huweza kuwa na uhusiano wa athari za ajali iliyompata mtu muda mrefu ama miaka kadhaa.

Kama kawaida, wanasayansi wapo kwenye tafiti mbalimbali juu ya madhara hayo na hivi karibuni wamekuja na jipya.

Hili ni kundi la wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Tiba Washington, Marekani pamoja na Chuo Kikuu cha Tiba Milan, Italia wameweza kutambua jinsi maradhi haya yanavyotokea.

Baada ya pekenyupekenyu zao walibaini kuwa hali hiyo inatokana na mabadiliko ya aina fulani ya protini kwenye ubongo inayojulikana kama amyloid beta.

Wao walibaini kuwa uzalishaji wa aina hii ya protini unapopungua unaongeza uwezekano wa kupatwa na maradhi hayo na inapozaliswa kwa kiwango kinachotakiwa, basi uwezo wa mawasiliano unakuwa katika hali nzuri.

Katika kuendesha utafiti huo, walichukua umajimaji uliopo katikati ya seli za ubongo kwa mtu mgonjwa ambaye alikuwa katika hali mbaya ambayo inahitaji kuwa na usaidizi wa karibu wa madaktari.

Majaribio hayo waliyafanya kwa watu 18 tofauti ambao ndugu zao walitoa ruhusa kwa madaktari hao kufanya hivyo kwa malengo ya utafiti.

Ndipo wakabaini uwepo wa aina hii ya protini lakini, ikabidi wajaribu kuona ni kitu gani kinachochochea kupungua amyloid beta wakati mtu akipata ajali hasa zinazohusiana na maeneo ya kichwa.

Kwa maneno mengine ni kwamba walijaribu kuchunguza kitu kinachosababisha mtu apate ajali, halafu awe amepona kabisa na kuendelea na shughuli zake lakini baadae ghafla maradhi haya yamkumbe.

Profesa David L. Brody wa Chuo Kikuu cha Washington ambaye alikuwa mmoja wa waandamizi kwenye utafiti huo, alisema kuwa kwa kawaida mgonjwa anakuwa tayari na maradhi hayo kabla hajapata ajali.

“Ajali inakuwa tu ni jambo ambalo linaharakisha dalili za ugonjwa huu na siyo kwamba yenyewe ndiyo inasababisha,” alisema Profesa Brody.

Lakini, anasema kuwa bado hawajajiridhisha katika utafiti huu kwa sababu bado kuna mambo ambayo wanapaswa kuyang’amua.

Hii ni pamoja na sababu zinazosababisha ajali kuchochea maradhi hayo na kwa maana kwamba kuathiri uzalishaji wa amyloid beta.

Utafiti wa wanasayansi hao unalenga zaidi katika kuweza kupata dawa muafaka kwa ajili ya kutibu maradhi haya.

Kwa sasa hakina tiba ya moja kwa moja bali madaktari hujaribu kupunguza athari zinazoandamana na maradhi.

Mara nyingi, tiba hii huwa na mafanikio mazuri kwenye hatua za mwanzo za maradhi hivyo tafiti za wanasayansi hawa huenda zikaja na uwezo wa kuzuia na hata kutibu kwa uhakika kwa wale ambao tayari wameathirika.


00000000000000

Utajisikiaje ukigundua gari unalotanua nalo mkeo alihongwa?


WASOMAJI wangu karibuni tena katika safu muipendayo ya Pasua Kichwa, wiki hii nina kitu kingine cha kupasua bongo zenu kisawa sawa.
Kuna jamaa mmoja alikuwa anaishi mitaa ya Ilala, mshikaji tulikuwa tunamuita baharia kwa sababu alifanya sana kazi hiyo zamani katika nchi mbalimbali za Ulaya.
Labda ndugu au jamaa zake wa karibu tu ndio walijua sababu ya kwanini, Baharia alirudi Tanzania na kuendesha maisha kupitia biashara ya nguo na vipodozi.
Jamaa alikuwa na roho nzuri kwa majirani zake na katika kushirikiana kwake na watu mbalimbali, ndipo siku moja akajikuta anamtongoza msichana mmoja wa maeneo ya Kinondoni.
Msichana huyo alikuwa anafanya kazi hoteli moja ya kifahari katika jiji la Dar es Salaam na huenda alikuwa miongoni mwa wakubwa kutokana na gari ya ofisi kumfuata na kumrudisha.
Baharia na msichana huyo wakawa hawakauki machoni mwetu pale mitaa ya Ilala.Wambeya na wakware wa ngono walimmezea mate sana msichana huyo kutokana na kuwa na umbo la kuvutia.
Siwezi kukwambia umbile lake lilivyo ila mitaani baadhi ya vijana hupenda kuwaita wanawake wa kuchora. Yaani paja paja kwelikweli, guu usiseme,kihuno namba nane, shingo kama ya twiga. Nadhani wengi mtakuwa mmeona michoro ya wanawake wa aina hiyo kwenye majarida ya kibongo.
Msichana huyo baada ya kuzama kwenye penzi la Baharia karibu mwaka mmoja, hatimaye wakafunga ndoa.
Kila mmoja alibaki na shughuli zake na mara mwanamke akaanza kubadilisha magari kama njugu. Mara kaja na Toyota Cresta, Sprinter, Suzuki, Prado, Benzi na mengine tele.
Binadamu hakosi wivu. Ghafla Baharia akaanza kuwa mbogo kwa mkewe na hata kufikia kumdunda hadi kumtoa manundu pale alipojibiwa vibaya au kutoridhishwa na majibu ya mkewe.
Jamaa alikuwa anamuuliza mke wake magari hayo ya nani mwanamke anasema yapo aliyonunua kwa fedha zake na aliyopewa na wazazi wake na mengine ya ofisini kwao.
Akiomba nyaraka ili kuthibitisha umiliki hapewi na mwishowe wanaishia kugombana na kupata suluhu wenyewe.
Baharia alikuwa mkali wee mwishowe akalainika kwa kuzingatia alikuwa anaumia roho sana kila alipokuwa anaambiwa atoe talaka kama anaona hayo magari yanamtia wazimu.
Basi akajikuta naye anaendesha moja kati ya magari hayo na siku hiyo Baharia akiwa mitaa ya Magomeni alisimamishwa na jamaa mmoja.
Mwenyewe alijua ni miongoni mwa watu anaojihusisha nao kibiashara,ile kushuka tu kwenye gari akaambiwa kwa sauti kali atoe funguo kabla hajakwenda kulala jela.
Baharia akagoma na kumwambia jamaa ni jambazi, kauli hiyo iliamsha hasira za huyo jamaa na kuanza kumsemea mbovu mwanaume mwenzake.
"Wee nini, hili ni gari langu kama mwanamke wako amekwambia lake kakuficha, leta funguo zangu siwezi kuhonga mwanaume mwenzangu," jamaa alimbwatia Baharia.
Zogo likajaza watu hadi polisi wakafika na kuamua kuwapeleka wahusika kituoni ambako jamaa alikabidhiwa gari lake baada ya kuonyesha nyaraka mbalimbali.
Baharia akawekwa selo ili kutoa maelezo polisi alilipataje, ndugu zake ndio walikwenda kumwekea dhamana akatoka na kurudi nyumbani kwake Ilala kwa daladala, je kama ingekuwa wewe ungefanyaje? tuma katika namba 0777 167514.


00000000

Thursday, September 25, 2008

• Kinyonya kuzikwa Shinyanga kesho

• Kinyonya kuzikwa Shinyanga kesho


Na Mwandishi Wetu

MAZISHI ya mwandishi wa habari wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd (UPL), inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, Ramadhan Kinyonya, yanatarajiwa kufanyika kesho mkoani Shinyanga.
Taarifa iliyotolewa na familia ya marehemu jana ilisema mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kesho asubuhi kwa ndege ya Shirika la Ndege la Precision kwenda Shinyanga na mazishi yamepangwa kufanyika jioni.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa leo saa 7.00 mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
Kinyonya (40), alifariki dunia juzi saa 7.00 mchana katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu tangu wiki iliyopita.
Alifikishwa hospitalini hapo kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu.
Kinyonya alijiunga na UPL mwaka jana baada ya kufanyakazi katika magazeti ya Mtanzania, Majira, Mwananchi na Champion.
Hadi mauti yalipomfika, Kinyonya alikuwa mwajiriwa wa UPL, akiwa mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Uhuru.
Kinyonya alizaliwa mwaka 1968 mkoani Shinyanga. Alisoma shule za msingi na sekondari mkoani humo hadi mwaka 1987 alipomaliza kidato cha nne.
Baadaye alijiunga na mafunzo ya upigajipicha, uandishi wa habari na kompyuta ngazi ya cheti.


00000000000