Thursday, October 30, 2008

funga mwaka ya wakenya na udugu wa gundi kwa obama


Obama akishinda atalifikia vipi boma?

wabunge wataka uwanja wa kisasa kwa Air Force One, mpya hii!

Wengi wanatazamia huenda Obama akawa akiitembelea Kenya mara kwa mara akiwa Rais wa Marekani

Wabunge wa nchini Kenya wametoa mwito wa kufanyiwa ukarabati haraka uwanja wa ndege wa Kisumu, ili ikiwa Barack Obama atashinda uchaguzi wa rais nchini Marekani, ataweza kuitembelea nchi hiyo kwa urahisi, ambayo ni nchi ya asili ya babake.
Wabunge wa jimbo la Nyanza huko magharibi mwa Kenya wanataka uwanja wa ndege mjini Kisumu upanuuliwe ili ndege ya rais wa Marekani iweze kutua hapo.

Babake Barack Obama ni kutoka katika kijiji kilicho karibu na hapo.

Ijapokuwa Barack Obama hajawahi kuishi Kenya, lakini ameshatembelea nchi hiyo mara tatu.

Waziri wa usafiri wa Kenya, Bw Chirau Ali Mwakwere amesema mpango wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kisumu hautamalizika hadi Julai mwaka 2010.

No comments: